Wednesday, May 2, 2012

Ijue idara ya USALAMA WA TAIFA...(III)

Habari News Tanzania


Idara ya Usalama wa Taifa (Tanzania Intelligence and Security Service) ndiyo idara maarufu na inayoogopwa sana na wananchi walio wengi. Kutokana na kutoifahamu vizuri idara hii, wananchi wengi wanaichukia na kuiogopa kwa kudhani kuwa hii ndiyo idara inayotumika katika kuwaua na kuwatesa watu wenye mlengo na mawazo tofauti ya kisiasa hususan viongozi wa vyama vya upinzani. Kwa mfano,  katika hali isiyo ya kawaida idara hii ilitajwa  sana na kuhusishwa na vifo vya aliyekuwa katibu mkuu wa CCM, marehemu Horace Kolimba, aliyekuwa waziri wa mipango na uchumi wakati wa serikali ya wamu ya pili  Profesa Kigoma Ali Malima, na hata mzee Mahimbo aliye fariki hivi karibuni kwa ajali ya gari. Hata hivyo hakuna ushahidi wowote unao onesha au kuthibitisha kwamba idara hii ilihusika kwa namna moja au nyingine na vifo hivyo.


Naibu Mkurugenzi Jacky Nzoka
Idara ya usalama wa Taifa (TISS) imeundwa kwa sheria ya bunge namba 15 ya mwaka 1996 (Tanzania Intelligence and Security Service act No. 15 of 1996) iliyosainiwa na Rais Benjamin Mkapa tarehe 20 mwezi Januari mwaka 1997. Sheria hiyo ndio inayoipa mamlaka Idara ya Usalama wa Taifa kufanya kazi zake ndani na nje ya jamhuri ya muungano wa Tanzania, na pia  ina ainisha majukumu, mamlaka na mipaka ya idara ya usalama wa Taifa. Kutokana na kuwepo kwa sheria hiyo siyo rahisi kwa idara hiyo kufanya mauaji ya raia wasio kuwa na hatia kwani idara itakuwa inavunja sheria na kukiuka mamlaka iliyopewa na bunge.

 Hata hivyo, kama ilivyo kwa jeshi la wananchi wa Tanzania na Jeshi la Polisi,  kadhalika idara hii INARUHUSIWA kutumia nguvu ya ziada (Reasonable force) katika kuwazuia maadui kumdhuru Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania, viongozi wengine na wananchi wote wa jamhuri ya muungano wa Tanzania. Kwa msingi huo, maafisa wa Usalama wa Taifa wanaweza kutumia nguvu au silaha yoyote inayofaa (reasonable force) katika kuwazuia magaidi, majasusi au maadui wanaotaka kufanya hujuma.
Hata hivyo nguvu hiyo ni lazima iwe inayofaa na isiyozidi kupita kiasi (reasonable force). Endapo adui atakuwa na silaha, basi maafisa wa Usalama wa Taifa watatumia silaha kumkabili adui hiyo. Ndio maana mtu aliyempiga kibao Rais mstaafu Ali Hassan Mwnyi hakuuawa kwa kupigwa risasi, bali alikamatwa na kushitakiwa.

Pamoja na idara hii kusajiliwa kisheria mwaka 1996, idara hii ilkuwepo tangu wakati wa utawala wa Mwalimu Julius Nyerere ambapo ilikuwa ikifanya kazi chini ya mwamvuli wa ofisi ya Rais. Pengine kitu kilicho pelekea kusajiliwa kwa idara hii ki sheria ni mabadiliko ya mfumo wa kisiasa na uchumi yaliyotokea  duniani mwishoni mwa miaka ya 1980 na kuingia Tanzania kwa kasi miaka ya 1990. Mabadiliko hayo na hasa kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi viliiweka idara hii katika hali ngumu ki utendaji kutokana na viongozi wengi wa vyama vya siasa kuamini kuwa idara hiyo ina kilinda chama tawala.

 Baadhi ya wakurugenzi waliopata kuongoza idara hii ni marehemu  Emilio Mzena (mkurugenzi wa kwanza) ambae alijipatia umaarufu mkubwa miongoni mwa wananchi kiasi cha kujulikana kwa jina  la 'Mr Serikali'. Wengine ni marehemu Dr Laurence Gama, Mzee Hans Kitine, marehemu Luteni Jenerali Imran Kombe, na Colonel Abson. Wakati wa uongozi wake Colonel Abson aliiboresha idara ya usalama wa Taifa na kuhakikisha muswaada wa kuundwa kwa  idara ya usalama wa Taifa kisheria unapelekwa bungeni na hatimae kusainiwa na Rais Mkapa. Hivi sasa Idara ya Usalama wa Taifa inaongozwa na Rashid Othman (Mkurugenzi mkuu) akisaidiwa na wakurugenzi wengine wanao ongoza kurugenzi ndogo.

Majukumu ya idara ya usalama wa Taifa.

Ni jukumu la idara  hii kumchunguza mtu yeyote, kikundi cha watu au taasisi yoyote endapo idara hiyo inayo sababu ya kuamini (reasonable cause) kwamba mtu huyo anahatalisha au ni chanzo cha hatari kwa usalama wa Taifa. Kwa sababu hiyo idara hii inaruhusiwa kuingia (kumchunguza) kwa mtu yeyote, idara yoyote ya serikali, mamlaka yoyote, polisi au 'policing organisation' yoyote.

Kukusanya taarifa za ki intelejensia na ki usalama, kuzichambua na kuzitumia taarifa hizo kuzuia vitendo vyovyote vya ki adui vinavyoelekezwa kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania. Kumshauri Rais na Mawaziri kuhusu maswala mbali mbali ya ki usalama. na kuvifahamisha vyombo vingine vya dola kuhusu uwezekano au kuwepo kwa vitendo vya ki adui katika jamhuri ya muungano wa Tanzania. Idara hii ndio iliyopewa jukumu la kuilinda jamhuri ya muungano wa Tanzania kutokana na vitendo vyote vya ki adui ikiwa ni pamoja na ujasusi (espionage),  uhujumu (sabotage) ugaidi (terrorism) na uhaini na uzandiki (subversion)

Kwa sababu hiyo, idara ya usalama wa Taifa inao wajibu wa kuilinda na kuitetea serikali ILIYO CHAGULIWA na wananchi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania ili isiondolewe madarakani KINYUME cha sheria. Idara inatakiwa kuwadhibiti watu au kikundi cha watu wanaopanga mapinduzi, wanaotoa vitisho au maneno ya kuwashawishi wananchi kuipindua serikali (uzandiki) au namna nyingine yoyote ya kuiondoa serikali pasipo kupiga kura kama inavyo agizwa na katiba ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.


DCI Robert Manumba
 Aidha idara hii inao wajibu wa kuzuia vitendo vyote vya kigaidi (terrorism) vinavyopangwa kufanyika katika ardhi ya Tanzania bara, Zanzibar na sehemu nyinginezo ambazo ni mali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania ( k.m barozi zetu). Idara inawajibika kufanya uchunguzi, kuwatambua magaidi, na kuvifahamisha vyombo vingine vya dola ili kupanga mikakati ya kuwakamata na kuwafikisha mahakamani.

Idara hii pia inalo jukumu la kuchunguza, kugundua na kuzuia njama zozote zinazopangwa na mtu binafsi, kikundi cha watu, au nchi jirani zenye lengo la kuleta machafuko, mauaji au maangamizi ya aina yoyote kwa wananchi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa lengo la kujipatia mafanikio ya kisiasa, ki uchumi, au kijamii ndani au nje ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Idara ya usalama inatakiwa kuwatambua watu wanaopanga mipango hiyo na watu au serikali zinazo wasaidia katika kutekeleza mipango hiyo, Kuchunguza vitendo vinavyofanywa na serikali za nje, asasi zisizo za kiserikali na wageni ili kubaini njama zinazounga mkono au kusaidia vitendo vya kijasusi au hujuma katika nchi yetu.

Aidha ni wajibu wa idara ya usalama wa Taifa kuhakikisha kuwa wananchi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania wanaendelea kuishia kwa utulivu, amani na mshikamano kwa kuchunguza na kubaini matatizo mbali mbali yanayo wakabili wananchi na kuishauri serikali iliyopo madarakani namna ya kuondoka kero zinazo wakabili wananchi. 

Idara hii pia ndio yenye jukumu la kuwalinda viongozi wote wa kitaifa ikiwa ni pamoja na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania, Makamu wa Rais, Rais wa serikali ya baraza la mapinduzi Zanzibar, na wengineo ambao idara kwa sababu moja au nyingine itaona wanafaa kupewa ulinzi.

Aidha idara ya usalama wa Taifa inawajibika kukusanya taarifa zote za kiusalama ndani na nje ya nchi na kuishauri serikali (Rais) kufanya maamuzi mazuri na yenye faida kwa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Kutokana na majukumu ya idara hii, maafisa wa usalama wa Taifa wanalindwa na sheria na kwamba hawawezi kushitakiwa mahakamani kwa jambo lolote walilolifanya wakati wa kutekeleza majukumu ya idara ya usalama wa Taifa.

29 comments:

Anonymous said...

Je nafasi za kazi katika idara hii ya usalama wa Taifa zinatangazwa wapi? na ni kwa watu gani?

Anonymous said...

ninayo hamu au shauku kubwa mno ya kuitumikia nchi yangu ktk idara hii.bali sijuh vigezo,au jinsi ya kujiunga,

Anonymous said...

Idara hii ninandoto nayo sana kuifanyia kazi lakini sijajua taarifa za kujiunga

hellen Fuko said...

nina hamu sana ya kufanya kaz katika idara hii naweza vipi kuungana na nyie

Unknown said...
This comment has been removed by the author.
Anonymous said...

ok,pongezi kwa idara ya usalama

Anonymous said...

usiweke picha

cleverobed said...

nina hamu,amasa, moyo, na upendo na wizara ya usalama wa Taifa kwasababu ninaipenda nchi yangu Tanzania kwahiyonina shauku ya kufanya kazi katika wizara hii
na sasa nimeanza kujiungz na jeshila kujenga Taifa ila ndoto zangu ni kufanya kazi katika wizara ya mambo ya ndani hususani usalama wa Taifa

Anonymous said...

HONGERA TISS

Anonymous said...

Bado idara hii ya usalama wa taifa inaupungufu wa informants katika ngazi za chini za kiutawala! binafsi nimejaliwa kuwa na hisia kali za kuweza kulitambua jambo kabla halijatokea na kama kuna jambo lishatokea huwa ni mwepesi na mtulivu ktk kutafuta kiini cha tatizo na kushauri nini kifanyike! mimi mzalendo raia wa jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Anonymous said...

Je, matukio mnayohusishwa nayo kama lile la kutekwa na kuteswa kwa m/kiti wa madaktari, Ulimboka pia m/kiti wa jukwaa la wahariri ndugu Kibanda, ni kweli mmehusika nayo kwani kazi zao zinaigusa Serilali moja kwa moja? Napenda kufahamu kihusu hayo

Mbele said...

Ilikuwaje idara hii haikuwajibika katika suala la watu kutuibia mamilioni ya fedha kutoka benki kuu? Je, wizi huu haukuwa hujuma ya wazi dhidi ya Tanzania? Nakumbuka Nyerere alikuwa macho sana na wahujumu uchumi, hata kama hapa na pale alizidisha mambo. Lakini leo je, idara hii imechukua hatua zipi dhidi ya hao walioiba benki kuu? Ningependa kupata maelezo, maana kwangu ni kitendawili.

Anonymous said...

Mnatekeleza wajibu wenu kwa asilimia kathaa ongezeni jitiada kukabiliana na wavunja sheria

Unknown said...

thanks for information

Anonymous said...

Mimi ni meja wa jeshi(jwtz) kwa imani yangu ninavyojijua nina vigezo vya kuitumikia nchi yangu kupitia idara hii. Nina ndoto hizo toka zamani lakini sehemu ya kuanzia sina.ninaomba nielekezwe kujiunga kama itakubalika.nahofia kuweka contacts zangu hapa emails kwa kuwa naamini kwa sasa si vema. Nipeni nafasi nitumikie nchi yangu kwa huo nao pia kama ninavyotumikia upande niliopo sasa.

Anonymous said...

kwani si mnajuana mkuu, ungewauliza wao... kufikia ngazi ya umeja wa jeshi nina imani una abc za hao jamaa.

Anonymous said...

Naitwa getrude,hongereni kwa kazi nzuri,nimekuwa nikitamani kuwa mmoja wenu toka nikiwa darasa la saba hadi sasa nimemaliza chuo na nipo na mambo yangu sijafanikiwa.kama kuna uwezekano wa kuwa mmoja wenu basi,naomba info kutoka kwenu kwenye email address yangu asseygetrude@yahoo.com.

Anonymous said...

hongereni kwa kazi mnayo ifanya(kulinda usalama wa nchi) napenda nami niwe miongoni mwa wafanyakazi wa usalama

Anonymous said...

Hongereni sana kwa kazi kubwa mnayoifanya kwa kulilinda Taifa letu zuri la Tanzania, HONGERENI, na mimi pia nimekuwa na ndoto hii ya kufanya kazi katika idara hii muhimu kwa Taifa letu, mimi kwa taaluma ni mtaalamu mifumo ya computer na mawasiliano yake, kama kuna utaratibu wa kujiunga na idara hii ningependa kujiunga nayo, kwa taarifa yoyote naomba nijulishwe kwa email hii:- rsrmtg@yahoo.com Nawapongeza sana kwa kila kazi mnayoifanya kama wajibu wenu kwa Taifa hili.

Unknown said...

Kujichomoza kwa mikono ya toka nje ya mashirika ya kijasusi kama FBI,M16 kunahatarisha idara yetu ya usalama kuweka siri zetu kwa nchi kama marekan kwani wanajipambanua na sera yao kama "wana maslahi ya kudumu na si urafiki au uadui" nadhani kama tungekuwa na idara ya usalama ya nje basi ingeweza tahadharisha idara ya usalama ya ndani ya nchi

Anonymous said...

Napeipenda sana idara hii yenye kazi ngumu hasa nyakati hizi za utandawazi.

Anonymous said...

Big up TISS

Anonymous said...

all the best for the country

Anonymous said...

ILIKE MORE MORE TO BE AMONG OF THE INTELLIGENCE

Anonymous said...

I DESIRE TO BE YOUR WORK MATE. HOW CAN I GET CONNECTED WITH YOU?

Unknown said...

Watanzania wengi sana tunahamu ya kuitu mikua nchi yetu lakini vigezo na jinsi ya kujiunga ni tatizo mfano mimi naomba kupatiwa maelezo

Anonymous said...

Mbona author hajibu hoja za wachangiaji hasa jinsi wanavyowapata wafanyakazi wapya?

Anonymous said...

Ninafanya degree ya philosopy naweza kufanya kaz mahali hapa?

Anonymous said...

Mimi nimebahatika kuona utendaji wa idara hii ktk nyakati zote za viongozi waliopita ..nidhamu sasa hivi hakuna maafisa wanajitangaza kwenye bar..kwamba wao ni kina nani it is pathetic. ..intelligence officer anatakiwa kuwa kama ghost